Back to repertoire
Swahili
Nitakwenda Mimi Mwenyewe
Copyright status has not been confirmed, so files are restricted to choir members.
Lyrics
Nitakwenda mimi mwenyewe, nikatoe sadaka kwa Bwana
{Aliyeniumba mimi, aliyeniumba mimi, aliyeniumba mimi
Mungu wangu, Mungu wangu, Mungu wangu
Kwa kuniumba hadi nikapendeza } *2
1. Kaniumba kwa mfano wake, kuliko viumbe vingine
Na sasa nikatoe shukrani
2. Vyote nilivyo navyo ni vyake, nimrudishie kwa mapendo,
Na sasa nikatoe shukrani
3. Mema mengi amenijalia, ya mbinguni na duniani
Na sasa nikatoe shukrani
4. Siku zote wanilinda vyema, wanitunza na kunijali
Na sasa nikatoe shukrani.
Liturgical seasons
Mass parts
Offertory