Moyo Wangu Wamtukuza Bwana
Copyright status has not been confirmed, so files are restricted to choir members.
Lyrics
(Moyo) Moyo wangu wamtukuza Bwana
(Roho) Roho yangu inafurahi *2
1. Kwa kuwa amemwangalia, kwa huruma mtumishi wake,
Hivyo tangu sasa watu wote, wataniita mwenye heri.
2. Kwa sababu Mwenyezi Mungu, amenitendea makuu,
(Jina lake ni takatifu) *2
3. Huruma yake ni kwa wote, wote wale wanaomcha,
(Vizazi hata na vizazi) *2
4. Huyatenda mambo makuu, kwa nguvu za mikono yake,
(Wenye kiburi hutawanya) *2
5. Hushusha wote wenye vyeo, kutoka vitini vya enzi,
Nao wote wanyenyekevu, wote hao huwainua
6. Huwashibisha wenye njaa, na matajiri huwaacha,
(Waende mikono mitupu) *2
7. Huilinda taifa lake, teule la mtumishi wake,
(Hukumbuka huruma yake) *2
8. Kama alivyowahidia, babu zetu kuwasaidia,
(Ibrahimu na uzao wake) *2
9. Atukuzwe Baba na Mwana, naye Roho Mtakatifu
Leo kesho hata milele, kwa shangwe milele Amina.