Back to repertoire
Swahili

Misa Mchanganyiko

Copyright status has not been confirmed, so files are restricted to choir members.

Lyrics

Gloria

Utukufu juu mbinguni kwa Mungu,
Na amani duniani kwa watu.
1. Tunakusifu, tunakuheshimu, twakuabudu na kukutukuza.
2. Twakushukuru, mwenye utukufu, mfalme wa mbingu, Mungu Baba yetu.
3. Ee Bwana Yesu, Mwana wa pekee, uliye Mwana kondoo wa Mungu.
4. Mwenye kufuta dhambi za dunia, ‘tuhurumie, utusikilize.
5. Unayeketi kuume kwa Baba, u peke yako Mkuu, Yesu Kristu.
6. Pamoja naye Roho Mtakatifu katika utukufu wake Baba.

Sanctus

Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu wa majeshi.
Mbingu na dunia zimejaa utukufu wako
Hosana juu, Hosana, hosana juu mbinguni
Mbarikiwa mwenye kuja kwa jina la Bwana.
Hosana juu, Hosana, Hosana juu mbinguni

Kyrie

Ewe Bwana, Bwana, Bwana Ewe Bwana *2
Ewe Bwana, utuhurumie *4
Ewe Kristu, Kristu Kristu ...
Ewe Bwana, Bwana, Bwana...

Liturgical seasons

Mass parts

Gloria
Sanctus
Agnus Dei