Back to repertoire
Swahili

Hodi Hodi Nyumbani

Also known as: Hodi Hodi

Copyright status has not been confirmed, so files are restricted to choir members.

Lyrics

Hodi hodi nyumbani mwako Bwana, ninabisha nifungulie
Nimekuja nyumbani mwako leo, nimekuja kukuabudu,
Kwa unyenyekevu naijongea, meza yako yenye baraka
Nakuja na sala zangu Ee Bwana, nakuomba zisikilize
Ninakutolea sadaka safi, Mungu Baba uipokee.

1. Nyua za Bwana zapendeza, zinapendeza macho kama nini
Natamani kuingia hekaluni, nikamwabudu
2. Nimeingia hekaluni, nimeingia hekaluni mwako
Nimekuja kuabudu kusujudu, nyumbani mwako
3. Unipokee Mungu wangu unitakase, mimi mwenye dhambi
Nimekuja mbele zako Mungu Baba, unipokee

Liturgical seasons

Mass parts

Entrance