Back to repertoire
Swahili
Bwana Unisafishe
Copyright status has not been confirmed, so files are restricted to choir members.
Lyrics
1. Mwana wa Mungu, Yesu Kristu,
Bwana ninakuomba unisikie.
Mimi mdhambi ninatubu.
Bwana unisafishe na damu yako.
Bwana unisafishe,
hakika sina wema (sina wema),
Bila neema yako,
mimi mwenyewe sina uwezo *2
2. Nina imani kwako Bwana, vile ulinifia msalabani.
Ulichukua dhambi zangu, Ukanifungulia kwako mbinguni
3. Mungu wa amani na mapendo, mimi nitatukuza jina lako kuu
Unishike mkononi, kazi yake shetani kutupoteza
4. Na kazi yangu ikiisha, Bwana ninatamani kuja kwako juu,
Niwe pamoja na wateule, tukitumikia mpaka milele.
Liturgical seasons
Mass parts
Entrance
Recessional